Zaidi ya wanafunzi 250 wanufaika na elimu ya utunzaji wa mazingira

Zaidi ya wanafunzi 250 wanufaika na elimu ya utunzaji wa mazingira

Na Christina Haule, Morogoro

ZAIDI ya wanafunzi 250 wa shule ya sekondari Uwanja wa Taifa iliyopo Manispaa ya Morogoro wamenufaika na elimu ya utunzaji wa mazingira waliyopewa na Taasisi ya wezesha mabadiliko (WEMA) inayowasaidia kulinda na kutunza mazingira ili kuwaepusha na magojwa ya mlipuko na ya kuambukiza kama vile kipindupindu.

Mkurugenzi wa Taasisi inayojihusisha na kutoa elimu kwa jamii (wezesha mabadiliko, WEMA) Dk.Lusako Mwakiluma alisema kufuatia ongezeko la magonjwa ya mlipuko kwa sasa kama vile U T I na kipindupindu yanayotokana na kuwepo kwa mazingira ya uchafu wameona waitumie nafasi hiyo kutoa elimu kwa wanafunzi hao ili kuifanya shule hiyo kuendeleza usafi na kuwa shule ya mfano kwa shule zingine za Manispaa ya Morogoro

Mkurugenzi huyo alisema pia wamewapatia vifaa mbalimbali vya usafi vyenye thamani ya shilingi milioni moja  ambapo alivitaja vifaa hivyo kuwa ni pamoja na mafagio , brashi za kusafishia vyooni, ndoo za kuwekea maji, plastiki za kuwekea takataka na dawa za kusafishia choo.

Alisema kupitia mradi huo waliouita kwa jina la ‘usiupotezee uchafu’ katika shule za sekondari sababu mazingira safi ni maendeleo ambapo mradi huo waliuanzisha baada ya kufanya tafiti na kubaini kuwa katika shule nyingi za sekondari za kata vyoo vyake ni vichafu ambapo kuanzishwa kwa mradi huo kutasaidia wanafunzi kutunza mazingira kwa kusafisha vyoo vyao kila siku ili kuepukana na magonjwa ya UTI na magojwa ya mlipuko kama kipindupindu.

Mwakiluma alisema wataendelea kutoa elimu katika shule zingine nane za Sekondari za kata na baadae kukagua kama wanaendeleza shughuli za utunzaji wa mazingira huku wakiazimia kutoa tuzo kwa shule itakayoendeleza suala zima la utunzaji wa mazingira.

“.Hatuwezi kuweka plasta kidonda bila ya kukiosha ndio mana tumetoa elimu hii ya utunzaji mazingira kwanza kwa kushirikiana nao kwenye usafi na baadae tukatoa vifaa vya kufanyia usafi” alisema Dk. Mwakiluma.

Naye Mwalimu wa nidhamu wa shule hiyo Asifiwe Charles  alisema vifaa vilivyotolewa na WEMA vitawasaidia wanafunzi kufanya usafi na kutunza mazingira vyema ili kuepukana na magojwa  kwani hapo awali kulikuwa na upungufu wa vifaa kama hivyo shuleni hapo.

Alisema awali shuleni hapo hapakuwa na dastibini za kuwekea  taulo za kike mara baada ya kutumika ambapo wasichana walikuwa  wakibadilisha pedi zao wanalazimika kutupa katika vyoo na kusababisha kuziba kwa vyoo mara kwa mara na kuingia gharama za kuzibua fedha ambazo zingetumika kwa maendeleo mengine ya shule.

Naye Dada Mkuu wa shule ya sekongari Uwanja wa Taifa Irene Mkondya  alisema ataendelea kuwahamasisha wanafunzi wenzie kutunza mazingira kwa maendeleo kwani ameweza kujifunza hasara za kuharibu mazingira kama kutupa taka hovyo kunavyoleta magojwa ya mlipuko kama kuharisha na kipindupindu hivyo aliwasasa wanafunzi wote kutunza mazingira kwani kwa kutunza mazingira watapata maendeleo.

Naye Omari Shabani mwanafunzi wa kidato cha tatu katika shule hiyo alisema  elimu waliyopata ya utunzaji wa mazingira itawasaidia katika maisha yao ya kila siku wawapo mashuleni na hata majumbani kwa sababu wanaweza kutunza mazingira kwa maendeleo.

Hivyo aliwasihi wanafunzi kuendelea kutunza mazingira ili kuepukana na magojwa ambayo yanaweza kuwakalisha chini na kuwafanya kushindwa kuendelea na masomo lakini pia kushindwa kuendelea na shughuli zao za maendeleo hapo baadae wakiwa wameshaanza kazi.

Taasisi ya wezesha mabadiliko hutoa elimu ya kujitambua  kwa vijana na wanafunzi, elimu ya afya ya uzazi, jinsi ya  kuepuka mimba na ndoa  za utotoni na jinsi ya kuepuka TB, Ugonjwa wa  upungufu wa kinga mwilini(UKIMWI) na kwamba kwa sasa inatekeleza mradi wa miezi nane katika shule 8 za sekondari za kata zilizopo manispaa ya Morogoro.

HAFLA YA UGAWAJI WA TAULO ZA MTOTO WA KIKE KATIKA SHULE ZA SEKONDARI MANISPAA YA MOROGORO KWA WANAFUNZI WANAOISHI KATIKA MAZINGIRA MAGUMU

HAFLA YA UGAWAJI WA TAULO ZA MTOTO WA KIKE KATIKA SHULE ZA SEKONDARI MANISPAA YA MOROGORO KWA WANAFUNZI WANAOISHI KATIKA MAZINGIRA MAGUMU

HAFLA YA UGAWAJI WA TAULO ZA MTOTO WA KIKE KATIKA SHULE ZA SEKONDARI MANISPAA YA MOROGORO KWA WANAFUNZI WANAOISHI KATIKA MAZINGIRA MAGUMU

a

AFISA MAENDELEO YA JAMII NA MRATIBU WA DAWATI LA MAENDELEO YA MTOTO MANISPAA YA MOROGORO , JOYCE MUGAMBI, AKIZUNGUMZA KWA NIABA YA MKURUGENZI WA MANISPAA YA MOROGORO KATIKA HAFLA YA UGAWAJI WA TAULO ZA MTOTO WA KIKE KATIKA SHULE ZA SEKONDARI MANISPAA YA MOROGORO KWA WANAFUNZI WANAOISHI KATIKA MAZINGIRA MAGUMU.

HAFLA HIYO IMEFANYIKA MEI 21 /2022 KATIKA UKUMBI WA MIKUTANO WA KILAKALA SOKO KUU LA CHIFU KINGALU MOROGORO.

TAULO HIZO ZIMETOLEWA NA TAASISI YA WEZESHA MABADILIKO CHINI YA MKURUGENZI WAKE DR. LUSAKO MWAKILUMA.🙏🏻🙏🏻🙏🏻🔥🔥🔥

JINSI YA KUJITAMBUA MWENYEWE

JINSI YA KUJITAMBUA MWENYEWE

Kama binadamu unatakiwa ujitambue  ili uweze kwenda na wakati au kufanya yale ambayo yanatakiwa  kufanyika  na yale ambayo hayatakiwi kufanyika usiyafanye.

Kuna mambo  ya msingi ya kuyafanya  ili uweze kufikiria  vizuri  wakati wote.  Na kila mtu atakayekuona  atajua huyu mtu amejitambua na amejua  umuhimu wake katika jamii inayomzunguka kwani utajikubali  wakati wote  na kuwaheshimu wengine.

Moja

Fikiri vizuri (jenga mfumo wa kufikiri vizuri); mfumo huu uwe endelevu; siyo usubiri upate tatizo ndiyo uanze kufikiri  vizuri  (usiwe kama zima moto).  Hii itakusaidia  kuanza kupanda mbegu njema kwenye mawazo yako ya kina ili maisha yako ya baadaye  yawe mazuri; yatoe mbegu nzuri/njema.

Mbili

Rudisha mawazo yako nyuma, jenga picha  yako ya utotoni.  Chagua taswira moja wakati ulipokuwa mtoto jione kimwili, kimavazi na mazingira ulipokuwa (nyumbani /shuleni au popote).  Kisha rudi kwako sasa hivi ukiwa mtu mzima; jione kama ulivyo sasa hivi ukiwa unamtazama huyo mtoto ambaye  umemjengea taswira; mtoto ambaye pia ni wewe.  Mtazame  na zungumza  naye, mwambie ulidanganywa kwamba ni mbaya; huna akili, huna thamani, huwezi, hufai nk; na wewe  uliamini kwa sababu ulikuwa mtoto.  Lakini sasa umekuwa mkubwa; fahamu ukweli halisi kwamba wewe ni mzuri, una akili unaweza na una thamani  sawa na wengine; unaweza na unafaa.  Rudia zoezi hili mara kwa mara; kila wakati hakikisha  unachagua  eneo ambalo  uliambiwa  huwezi; Futa  imani zote mbaya kwenye mawazo yako ya kina.

Tatu

Ni ile ya kufanya zoezi la kurudia rudia maneno pamoja na kujenga taswira  mfano: kila wakati  jiambie ninaweza; ninafaa; nina thamani, najiamini.  Imani ni muhimu sana wakati unajimbia maneno hayo.

Nne

Hapa utaenda kutumia mshumaa, uwashe mshumaa; uweke mbele yako juu ya meza au stuli au sehemu yoyote.  Angalia ile sehemu  ya mshumaa inayowaka moto (siyo mshumaa wote) kwa muda wa dakika 10, 30 au zaidi.  Baada ya hapo fumba macho yako yote ili uuone ule moto wa mshumaa  kwa kutumia macho yako ya akili (yaani jicho la tatu).  Utaenda kuona moto huo ukiwa wa kijani, bluu, njano au mweupe.  Baada ya kuuona, anza kuchoma zile tabia  au mambo  yanayokukera au kuwakera  wengine mfano: Choyo, wivu, uzinzi, dharau, zichome  moja baada ya nyingine.  Wakati unazichoma utaona moto wa mshumaa ukiongezeka  ukubwa au utaona moshi.  Fanya zoezi hili mara kwa mara. Baada ya muda utashangaa kuona tabia au mambo hayo yamekwisha na tabia hizo umeziacha kabisa.

Tano

Ni ile hali ya kutumia kioo, simama jitazame kwenye kioo ikiwezekana kila siku asubuhi na jioni.  Tafuta zile kasoro ambazo uliambiwa  na jiambie kwamba huna.  Kama uliambiwa wewe ni mbaya; Basi jiambie wewe ni mzuri, huku ukijiangalia bila kujiogopa kwenye kioo.  Lakini kama uliambiwa huwezi, jiambie naweza sana.  Pia jikubaai kama ulivyo na jiambie umekamilika, una thamani na unastahili.

Sita

Ni ile hali ya kupata nafasi ya kuyapa mawazo yako ya kawaida  baada ya kupewa nafasi ya muda  hatimaye yatachukuliwa mawazo yako ya kina, mambo haya  mapya  yataua au kukausha ile miche/miti iliyoota  kwenye mawazo  yako ya kina; miti hii ni ile ya mambo ambayo yanakukera au kuwakera wengine. Kwa ile ambayo imeshazaa matunda haiwezi kukauka kwani umeshaanza kuvuna kitu ambacho nidyo maisha unayoishi hivi sasa.  Njia hizo zote tano ni za mzunguko.  Hii ya sita  ni ya njia ya mkato kwani unaenda moja kwa moja  kwenye mawazo yako ya kina na kuyaambia yale unayoyahitaji ambayo ni kinyume na yanayokukera.

Nguvu ya uumbaji kitaswira  na kujipa nguvu

(i)                 Kumbuka: Imani – hisia- matokeo

(ii)               Ondoa mipango ya zamani kwenye  mawazo ya kina ndiyo sababu ya msingi ya kukwama kwani nyuma ni historia na inatia uchungu ukiifikiria.

Kuna aina tatu ya uumbaji  kitaswira: sauti, kuona na hisia.

(iv)             Kila mmoja ana aina yenye kutawala kwake awe anajua au la.  Kuna wengine  wanatawaliwa  na aina mbili.  Katika matumizi ya uumbaji kitaswira, tunaanza na aina yetu, baadaye tunajifunza nyingine.

(v)               Ili kujua aina yako, jaribu kufikiria unachohitaji sasa hivi ili uone.  Mwanzoni unaweza kusikia  sauti inayokuambia hutaweza au ni mzaha ufanyao.  Unatakiwa ufanye  mazoezi  mengi ili uweze kujenga uwezo wako ulionao au uliopotea.

(vi)             Mawazo yako ndiyo  yenye  kukufanya/kukuwezesha ujenge uumbaji kitaswira.  Unachokiona kila siku ni matokeo ya kilicho  mawazoni kila siku. Hivyo, bila kujua huwa tunaumba yale tusiyoyataka maishani.  Uumbaji  kitaswira unawakilisha utunzaji wa mbegu (mawazo) kutegemea  ni mbegu gani tumepanda.

(vii)           Makosa  yajitokeza sana; usiweke  nguvu  kwenye kukosa, kwenye usichotaka na kwenye usichonacho.   Mfano: kama umepanga kwenye chumba  kimoja na unataka kujenga nyumba yako, usijiambie nimechoka  kukaa kwenye  haka kakibanda au maisha ya kupanga yamenichosha.  Sema lazima niambie nyumbani kwangu yaani nyumba niliyojenga mwenyewe.

(viii)         Unapokuwa  kwenye uumbaji  kitaswira, hisi au  ona kama vile jambo limeshakuwa  tayari – piga picha ya utayari wa jambo lako.

(ix)                                                                                   Jinsi ya kufanya (hatua);

(i)                 Tafuta mahali tulivu

(ii)               Tuliza mawazo yako

(iii)             Weka nguvu zako  za mawazo  katika jambo  unalolitaka

(x)                Simamia kufikiria vizuri wakati wote utakaokuwanao na utashangaa kuona matokeo mazuri na kwa muda mfupi sana.

Na: Lusako Mwakiluma

MWAKA 2022 UNA MAAZIMIO YAKE UMEAZIMIA NINI?

MWAKA 2022 UNA MAAZIMIO YAKE UMEAZIMIA NINI?
  1. Fanya mazoezi madogo madogo nyumbani kwako unapoamka 11.30asubuhi mpaka 12.00 asubuhi. Hii itakusaidia kuwa makini kichwani na mwilini, mwili unajengwa kwa fikra, mwili na akili yako.  Kama asubuhi yako itakuwa nzuri na chanya kila kitu kwa siku hiyo kitakuwa hivyo.  Jaribu sasa na utaona mabadiliko makubwa kwa mwaka huu mpya na mwenye nguvu zaidi kwako.
  2. Acha kuangalia simu yako mara unapoamka asubuhi, baada ya mazoezi ebu mtafakari Mungu wako na angalia leo itakuwaje kwa manufaa yako, familia na jamii inayokuzunguka, usipoteze muda kwenye simu hakuna jipya ila kupoteza yale uliyoyapanga. Simamia unachokiamini na tenda kwa wakati kulingana na nini kikamilike kwa siku hiyo.
  3. Tafuta chakula ambacho kitakuletea afya na nguvu pia usile bora kula hii itakuletea uzito mkubwa na kuharibu afya yako. Ukitembelea nyumba ya mtu usikaribie kila kilichoandaliwa fuata ratiba yako na fuata mlo kamili unaoutumia.  Unaweza kuwashirikisha huwa unatumia nini kuepusha kula kitu ambacho sio cha kujenga mwili na faida yako.
  4. Fanyia mazoezi kila siku kile kitu unachokipenda, mfano unataka kuwa kama Oprah Winfrey basi hakikisha kila siku unafanyia mazoezi maneno yake, matendo yake hata kama unaweza kuanzia kazi hicho unachokipenda itakujenga zaidia na utakuwa imara sana, kwani mazoezi mazuri ni yale ya kuyatendea kazi.
  5. Wafanyie watu yale ambayo unapenda kufanyiwa wewe na sivinginevyo, angalia usimuumize mtu baada ya hapo muhurumie na kumsaidia Yule mwenye shida. Dunia ni Karma kile kibaya utakachotenda kwa mwenzio kitarudi kwako kwa maumivu, kuwa makini na wale wanaokuzunguka tenda wema kasha nenda zako, wala usihesabu shukurani kutoka kwa mtu mlipaji sio wewe.

Naamini hiki ni chakula cha siku na mwaka mzima najua utashiba na mwaka 2022 hautakuwa wa hasara kwako.        Simamia njia tano ziweze kukubadilisha na kukufanya mpya wakati wote.

Dr Lusako Mwakiluma

Muinuaji na Mhamasishaji

WEMA- Yakabidhi Choo cha Mtoto wa Kike

WEMA- Yakabidhi Choo cha Mtoto wa Kike

Choo cha Mtoto wa Kike Shule ya Sekondari Uluguru ,kilichofadhiliwa na Taasisi ya WEZESHA MABADILIKO.

Mkurugenzi wa WEZESHA MABADILIKO, Dr. Lusako Mwakiluma (kushoto), akisalimia na Afisa Elimu Taaluma Msingi Manispaa ya Morogoro, Leah Selemani (kulia) mara baada ya uzinduiz wa Choo cha Mtoto wa Kike.

Mkurugenzi wa WEZESHA MABADILIKO, Dr. Lusako Mwakiluma (watatu kutoka kushoto) , Mtendaji wa Kata ya Kihonda Tatu Ally (kushoto) wakiwa na Wanafunzi mara baada ya uzinduzi wa Choo cha Mtoto wa Kike.

Mkurugenzi wa WEZESHA MABADILIKO, Dr. Lusako Mwakiluma (watatu kutoka kushoto),akimkabidhi ndoo ya kunawia maji Afisa Elimu Taaluma Msingi Manispaa ya Morogoro, Leah Selemani (kulia).

TAASISI isiyo ya Kiserikali ya WEZEESHA MABADILIKO chini ya Mkurugenzi wake. Dr. Lusako Mwakiluma,imeikabidhi Manispaa ya Morogoro Choo cha Mtoto wa Kike katika Shule ya Sekondari Uluguru.

Tukio hilo la makabidhiano ya Choo limefanyika hivi karibuni ambapo Choo hicho katika makabidhiano kilipokelewa na Mwakailishi wa Mkurugenzi kutoka idara ya elimu Msingi, Leah Selemani.

Akizungumza mara baada ya kukabidhi choo hicho, Mkurugenzi wa WEZESHA MABADILIKO, Dr. Lusako, amesema kwa kuwa wanawake wengi wamekuwa na changamoto nyingi katika mabadiliko ya kimwili hivyo wameona kujenga Choo cha Mtoto itakuwa ni suluhisho la kuwaondolea adha wanafunzi wakike wanapoingia katika hedhi.

Dr. Lusako,amesema kuwa tafiti  zinaonesha kuwa mtoto wa kike anakosa masomo siku 4 hadi 5 kila mwezi kutokana na ukosefu wa huduma ya vyoo bora na maji salama na safi shuleni ambapo Tanzania ni miongoni mwa nchi zilizosaini mkataba wa Malengo ya Maendeleo Endelevu ifikapo mwaka 2030. Miongoni mwa malengo hayo ni lile lengo namba 4: linalohamasisha kuhusu Elimu Bora, Lengo la 5: linalo hamasisha juu ya Usawa wa Kijinsi na lengo namba 6: kuhusu Maji Safi na Salama.

“Huu ni mwanzo tu bado tuna malengo ya kusaidia na shule nyengine ,  tunataka choo hiki kiwe cha mfano katika Manispaa yetu ya Morogoro , tuliona kuna Choo Tubuyu Sekondari lakini kuna chengine hakijaisha pale Kihonda Sekondari, sisi baada ya kuguswa na jitihada hizi, tumeona nasisi  tuunge mkono jitihada za  Manispaa yetu kwa kuwajengea Choo hiki cha Kisasa  ili kuhakikisha mtoto wa kike anawekewa mazingira rafiki anapokuwa shuleni ili aweze kuhudhuria siku za masomo kwa ukamilifu kama ilivyokuwa kwa mtoto wa kiume kwani “Ukimkomboa mtoto wa kike umekomboa Taifa zima” Ameongeza Dr. Lusako.

Aidha, amesema kuguswa kwao katika ujenzi wa Vyoo vya Mtoto wa kike imetokana na changamoto zinazoendelea kuwakabili wanafunzi kukosa vyoo bora na maji salama na safi shuleni. Tatizo hili linawaathiri watoto wa kike zaidi kwani wanashindwa kujistiri hasa wanapokuwa katika siku zao za hedhi katika mazingira ya shuleni.

Naye Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro,ambaye pia ni afisa Taaluma Msingi,  Leah Selemani, amempongeza Mkurugenzi wa WEZESHA MABADILIKO kwa  kuwasaidia wanafunzi wa kike shuleni.

Amesema Vyoo hivyo vitapunguza utoro kwa watoto wa kike kwani wengi wamekuwa wakishindwa kufika shule wakati wa hedhi lakini baada ya ujenzi huo utasaidia sana na wanafunzi watahuduhuria shule wakiwa katika hali hiyo maana ipo sehemu salama kwao katika kujisafisha na kujilinda.

Mama Selemani , ameowaomba Wazazi kuwahimiza watoto kwenda shule mara baada ya kupata hedhi kwani mabadiliko hayo yanazuilika wakiwa shuleni.

“Dada yetu Dr. Lusako, amefanya jambo zuri sana, sisi kama Manispaa tunampongeza sana kwa jitihada zake, hii ni mbinu nzuri sana , hiki ni choo cha 3 kwa Manispaa yetu, kimoja kipo Tubuyu Sekondari, kingine kipo Kihonda Sekondari hakijaisha na mategemeo yetu kiishe mwaka huu unaokuja wa 2022, choo hiki  kitasaidia kupunguza utoro kwa watoto wa kike wanaoingia katika siku zao (hedhi), kumekuwa na changamoto wanafunzi kubeba pedi kwenye begi na kwenda nazo shule wengine wanaenda kuomba ofisini , lakini kwa hali hii ni vigumu hata kutambua mtu yupo katika hali gani maana vifaa vyote vitakuwa chooni ni yeye kwenda na kujihudumia”Amesema Mama Selemani.

USIMKOPESHE RAFIKI AU NDUGU YAKO

USIMKOPESHE RAFIKI AU NDUGU YAKO

Kwa nini leo nimefikiria haya?  Naomba nikwambie pesa ni jawabu la mambo yote namadhambi yote yameanzia kwenye pesa.   Unaweza kuwa na rafiki au ndugu mliyeshibana sana lakini pesa ikaja kuwatenganisha kwa urahisi mno na mkachukiana milele.  Pesa inatengeza marafiki na pia inaleta uadui ndani yake.  Basi ili uishi kwa amani kila kitu unatakiwa ukifanye kwa kiasi.

Kila wakati fanya msaada wa kipesa kama zawadi usifanye kama mkopo.  Kama haujampa mtu  msaada wa kipesa urafiki wenu unaenda kuisha taratibu. Kama uko kwenye eneo la kuweza kumsaidia mtu basi msaidie usimkopeshe mpe tu.  Na kama unajua hauwezi kumpa usimkopeshe itaenda kukuumiza wewe mwenyewe

(Ron Henley).

Sababu ya kutompatia mkopo rafiki au ndugu wa karibu ni kwasababu ya kuondoa usumbufu usio wa lazima wa kudaiana pasipo mashiko. Uhusiano wenu unaenda kuvunjika kama sio kuharibika kabisa.  Sababu ya watu inayowapelekea kupata matatizo ya kipesa ni kutojua jinsi ya kufanya kazi na pesa au jinsi ya kutumia fedha.  Ukiwakopesha wala hawajui wanaenda kufanyia nini kwani hawajajiandaa cha kwenda kufanyia hizo pesa.

Kabla ya kufahamu hivyo watachukua pesa kwako tena wataanza kutoa udhuru wa kushindwa kukurudishia.  Kinachofuata hapo ni kukukimbia kila wanapokuona.  Kuacha kupokea simu yako na mwisho kutofungua mlango mara unapopiga hodi majumbani kwao.

Naomba kwa ushauri kama unataka kumsaidia ndugu yako au rafiki mpatie pesa kama msaada na sio mkopo ili uishi kwa amani kwani utakapomkopesha hiyo pesa usiihesabu katika akiba yako kwani imeondoka na hauwezi fahamu itarudi lini.

Hii ni kwa faida yako ya watu wengine.

Karibu tusaidiane pale tuliposhindwa na tunapoweza tuelekezane.

Kwani maarifa ni mali kuliko pesa.

Lusako Mwakiluma

Mhamasishaji na Muinuaji kwa waliokata tamaa na kuugua